PROFESA NDAKIDEMI AKAGUA UJENZI WA MADARASA SEKONDARI YA MASOKA

 


MBUNGE  wa Jimbo la Moshi Vijijini Profesa Patrick Ndakidemi  ameendeleza na ziara yake ya kutembelea jimbo hilo kwa kutembelea Kata ya Kibosho Kirima na kukagua miradi ya maendeleo iliyotekelezwa kwa kipindi cha mwaka mmoja uliopita tokea aingie madarakani.   




Miongoni mwa miradi aliyokagua ni pamoja na ujenzi wa madarasa mawili katika  Shule ya Sekondari ya Masoka yaliyojengwa kwa fedha za UVIKO 19 kwa thamani ya shilingi milioni arobaini.


 Akitoa ripoti ya mradi huo, Mkuu wa Shule Mwalimu Ahmed Litinji alieleza kuwa mradi huo umekamilika kwa asilimia mia moja.



 Mwalimu huyo aliwashukuru wananchi na viongozi mbalimbali kwa ushirikiano wao  mkubwa katika utekelezaji wa mradi pamoja na viongozi wa Kijiji cha Boro  kwa kuhamasisha nguvu kazi kwani ushiriki wao  umesaidia kupunguza gharama za ujenzi na muda wa utekelezaji wa mradi.



Mbunge alimpongeza Mkuu wa Shule  kwa mafanikio  makubwa aliyoyapata katika kukamilisha mradi kwa wakati, na maendeleo ya shule kwa ujumla. 




Diwani wa Kata ya Kibosho Kirima Inyasi Stoki Mushi  alimshukuru Mbunge kwa kutembelea Shule hiyo na amemshukuru kwa fedha za mfuko wa MAENDELEO wa jimbo (Tsh Milioni Tatu) ambazo zilitumika kuboresha miundombinu ya shule hiyo.

0 Comments:

Post a Comment