#UPDATES: POLISI WAMSAKA DEREVA WA LISSU

Dereva wa Tundu Lissu anonekana kwenye Picha hii akiwa ameshikilia nguo za Tundu Lissu muda mfupi baada ya kupigwa risasi Tundu Lissu.

 DEREVA wa Mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lissu, (CHADEMA), ametakiwa afike polisi  ili aweze kutoa maelezo kuhusiana na tukio  la kupigwa risasi bosi wake.

Aidha  Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dk Vicent  Mashinji anatakiwa kufika  kwa Mkuu wa Upelelezi, (RCO), wa Dar es Salaam au Dodoma  kutokana kauli anayodaiwa kuitoa akidai kuwa katika uchunguzi wao wamewabaini wahusika.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Dodoma, (RPC), Gilles Muroto kuwa mpaka sasa wamekata magari nane aina ya Nissan Patrol kwa ajili ya uchunguzi wa tukio la kupigwa kwa risasi kwa Rais huyo wa Chama cha Mawakili nchini, (TLS),  Lissu.

Amesema uchunguzi huo unafanywa kwa kuvishirikisha vyombo vingine vya Serikali ikiwemo  Mamlaka ya Mapato Nchini (TRA).

0 Comments:

Post a Comment