BREAKING: Askofu Mkuu wa Kanisa la P.A.G Tanzania aungana na Gwajima Sakata la Tundu Lissu

Askofu Mkuu wa kanisa la P.A.G Tanzania
Mh. Daniel Awet
Tangu kutokea kwa tukio la Kupigwa risasi kwa Mbunge wa Singida Mashariki na Rais wa Chama cha wanasheria Nchini Tanzania TLS Tundu Antipas Lissu, Viongozi Mbalimbali wa serikali, taasisi na viongozi wa dini wamekuwa mstari wa mbele kutoa maoni yao juu ya tukio hilo nakulaani.

Viongozi waliotoa masikitiko yao walikuwa pamoja na Rais wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania Mh.Dkt. John Pombe Magufuli na viongozi wengine pamoja na mastaa maarufu wa muziki nchini wakiongozwa na staa wa 'Eneka' Diamond Platnumz
Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima Bishop Dkt Josephat Gwajima 

Viongozi wa dini nao hawakua mbali katika kuguswa na tukio hilo la kupigwa risasi kwa Tundu Lissu ambapo Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima Bishop Dkt. Josephat Gwajima aliahidi kuongoza ibada Maalum kumuombea Tundu Lissu.

Sasa ikufikie taarifa kuwa VOA TV News na Habaritanzaniagracemacha.com zimempata Askofu Mkuu wa Kanisa la P.A.G Tanzania Askofu Daniel Awet ambaye pamoja na kulaani tukio hilo  alitoa wito wake kwa viongozi wa dini kuiombea amani nchini.

Hii video hapa chini kutoka VOA TV News ina kila kitu Play ushuhudie...

0 Comments:

Post a Comment