CCM watwangana

Wabunge wa CCM ambao wanahudhuria mkutano wa Bunge maalum la Katiba wameingia katika mgogoro na mzozo mkali wenyewe kwa wenyewe na kuamua hata kususa kuhudhuria vikao vya kichama (party caucus) kwa ajili ya kuweka misimamo.

Chanzo cha mkwaruzano wa wabunge hao ni kitendo cha vigogo wa chama hicho kuwateua Ole Sendeka, Peter Serukamba na Ummy Mwalimu kuwa ndio pekee watakuwa wakiwakilisha maoni na misimamo ya chama katika kipindi chote walichokuwa wakijadili rasimu ya kanuni za bunge hilo. Wale waliokuwa wakifuatilia bunge watakuwa wanalikumbuka swala hilo vema.

Hali hiyo imewafanya wabunge wengine wa CCM kuona kuwa wamepuuzwa na chama huku watatu hao wakitafutiwwa umaarufu wa nguvu kupitia kanuni hizo huku mambo mengi waliyoyaombea marekebisho yakitoka kwa Andrew Chenge na kuzungumzwa na watatu hao pekee.

Aidha watatu hao waliamua kula dili pia na mtumishi mmoja wa Bunge aliyetoka Baraza la wawakilishi Zanzibar kupenyeza majedwali ya mabadiliko kwa Mwenyekiti Kificho kabla ya Waziri wa sheria zanzibar ambaye ni mjumbe wa Kamati wa kamati ya kanuni kustukia dili hilo na kumwambia mwenyekiti kuwa baadhi ya mapendekezo yanayotolewa na akina Ole sendeka na Ummy hayakuletwa kwa wakati lakini yamepenyezwa kijanja. Uchunguzi ulifanyika na kubainika kuwa mtumishi huyo ndie aliyekuwa akitumiwa na akina Ole Sendeka na sasa mtumishi huyo amerejeshwa kwao Zanzibar.

CCM kwa sasa hawahudhurii kikamilifu vikao vya kichama na kuwaachia wabunge wachache na mfano mzuri ni kikao cha juzi ambacho kilihudhuriwa na wabunge wasiozidi 100 wa CCM huku wengine wakiweka mikakati yao binafsi ya kupinga mwenendo wa wenzao katika mkutano huu.

Hata swala la Kura ya siri au wazi ambalo limeachwa pending na kanuni, lilishindwa kufikiwa muafaka kwa sababu ya wanaCCM wengi kususia mikutano na kuwaacha Ole Sendeka na wenzake wakishikia bango kwa niaba ya chama na sasa wanategemea Rais JK ataukata mzizi wa fitna atakapokuja kuzindua bunge Ijumaa au Jumamosi wiki hii kwa kuzungumzia msimamo wake kuhusu aina ya kura na huo ndio unatarajia kuwa msimamo wa bunge pia hapo mbele ya safari.

0 Comments:

Post a Comment