IMAMU wa Msikiti wa Sawiyatu Qadiria, Hassan Bashir, (33)
amejeruhiwa vibaya usoni na kwenye bega la kushoto baada ya kumwagiwa
kimiminika kinachodhaniwa kuwa tindikali.
Amelazwa kwenye wodi ya majeruhi hospitali ya Mkoa ya
Mount Meru anakopatiwa matibabu, Imamu huyo alisema kuwa tukio hilo lilitokea
juzi kwenye majira ya kati ya saa 3:30 na saa 4:00 usiku maeneo karibu na
msikiti huo anauongoza maeneo ya Tindiga Unga Ltd.

0 Comments:
Post a Comment