GWAJIMA MGENI RASMI SIKU YA KIMATAIFA YA MWANAMKE WA KIJIJINI

 WAZIRI wa maendeleo ya Jamii Jinsia na makundi maalumu, Dkt Dorothi Gwajima,anatarajiwa kuwa mgeni rasimi kwenye kilele cha siku ya Mwanamke anayeishi Kijiji duniani itakayoadhimishwa Kijiji cha Olevolos kata ya Kimnyaki, Wilayani Arumeru Oktoba 15 .


Madhimisho hayo kitaifa yanafanyika Kijijini hapo kutokana na Kijiji hicho Nchini kuanzisha Sheria ya kutoa adhabu kwa kila mkazi atakae kiuka maadili ikiwemo kuvaa mavazi ya mlegezo maalumu kata K ,kunyoa kiduku watatozwa shilingi elfu 50.


Lengo la kuanzishwa Sheria hiyo ni kudumisha maadili yaliyo mema na kuweza kuwarejesha wale wote walioacha maadili kurejea kwenye maadili mema ambayo yatakuwa ni mfano wa kuigwa.



Akifungua  mafunzo maalumu yaliyoandaliwa na Jukwaa la Mwanawake Kijijini 2023 kwenye uwanja wa Kijiji cha Olevolosi kata ya Kimnyaki Wilayani Arumeru,Afisa maendeleo ya Jamii Mkoa wa Arusha,Blandina Nkini,amehimiza Jamii kuzingatia maadili Ili kuondoa mmomonyoko wa maadili ambao kwa sasa limekuwa ni tishio kubwa Kwa wananchi wa Vijijini na mijini.


Amesema chanzo cha mmomonyoko wa maadili  ni familia kuyumba na kushindwa kutimiza wajukimu na uwajibikaji  kuna sababisha mmomonyoko wa maadili hivyo iwapo familia zitasimama imara mmomonyoko huo hautakuwepo


Amesema kuwa  Wanawake ndio wazalishaji wakubwa lakini wamekuwa wakikandamizwa Kwa kunyimwa hali ya kumiliki mali na kushirikisha kwenye maamuzi.


Afisa usitawi wa Jamii Mkoa wa Arusha,Denis Mgie,amesema kuwa Kijiji hicho kimeweka Sheria hiyo baada ya kuwepo changamoto Katika malezi,hivyo Kijiji hicho kimekuwa Wakala mkubwa wa mabadiliko Katika malezi na makuzi ya watotonchini.


Amesema kuwa kauli ya kusema sitaki mtoto wangu  ateseke imetumika vibaya  siku tulizania  tumelea kumbe tumeharibu.


Amesema kuwa Jamii inatakiwa kuongoza Kwa misingi mizuri kwa kuweka misingi ya watoto na Vijana Ili kuelewa nafasi ya mzazi au mlezi .


Amesema mmomonyoko wa maadili pia unaochangiwa na baadhi ya wazazi au walezi kutokuwajibika  kulea watoto kwa kuacha jukumu hilo la kulea watoto kwa dada wa kazi na matokeo yake mtoto akiwa mkubwa atampeleka mzazi kwenye Kituo cha kulea wazee


Amesisitiza kwamba  malezi ya watoto ni nguzo muhimu Katika  kuelekea kuwa na taifa lenye watu wanaojitambu.


Kauli mbiu ya madhimisho hayo inasema Wezesha Wanawake wanaoishi Kijijini kwa uhakika wa chakula , lishena uendelevu kwa familia .

0 Comments:

Post a Comment