RAHA BEVERAGES NA TBL ZAMKOSHA NAIBU WAZIRI

 



SERIKALI yaridhishwa na uhifadhi na hatua zilizochukuliwa na kampuni ya Raha beverages limited inayozalisha mvinyo na Kampuni ya Bia nchini,(TBL) jijini Arusha, walivyoboresha mifumo yao ya maji taka hivyo kuwa salama kwa mazingira na afya za watu wanaozunguka viwanda hivyo.

 

Aidha wenye viwanda nchini wametakiwa kuhakikisha wanaweka mifumo sahihi ya kisasa  kudhibiti maji taka yanayotoka kiwandani na kuacha kuyaelekeza kwenye makazi ya watu hatua inayosaidia kuondoa uharibifu wa mazingira na kuleta madhara ya kiafya Kwa binadamu.

 


Naibu waziri, ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Hamad Hassan Chande ameyasema hayo leo alipotembelea kampuni ya Bia nchini, (TBL) na Kampuni ya Raha Beverages .

 

 

Naibu waziri akiwa ameambatana na viongozi wa NEMC Mkoani hapa,aliridhishwa na mfumo wa kudhibiti Maji taka unaotumiwa na viwanda hivyo ambapo huchakata maji taka na kuyarejesha upya kiwandani kwa ajili ya matumizi mengine ikiwemo umwagiliaji wa mimea jambo ambalo amevitaka viwanda vingine kuiga mfumo huo.

 

Akiongea wakati akikagua mtambo wa kuchakata Maji taka kiwanda cha Raha beverage, Naibu waziri, Chande aliridhishwa na na hatua ya kiwanda hicho kwa kuweza  kudhibiti Maji taka yasitiririke kuelekea kwenye makazi ya watu hivyo akavitaka viwanda vingine kujifunza kutoka kampuni hiyo.

 

Hata hivyo alisema ipo dhana kwa baadhi ya viwanda kuwa kutiririsha Maji taka ya viwandani kwenye makazi ya watu kwa madai maji hayo yamechakatwa na hayana madhara kwa binadamu na mimea jambo alilosema kuwa watatuma wataalam wao kwenye maeneo hayo wakafanyie  utafiti ili kujiridhisha .

 

"Tutatuma wataalamu wetu kwenye viwanda vinavyotiririsha Maji kwenye makazi ya watu  wakidai maji hayo  hayana madhara ili wafanye uchunguzi na Serikali itatoa tamko, yapo malalamiko mengi ya wananchi yanayohitaji majibu ya wataalamu,"amesema Naibu Waziri Chande. 

 


Kwa upande wake meneja wa mauzo na masoko katika kiwanda cha Raha Bereveges , Daniel Olomi amemweleza Naibu Waziri, Chande kuwa  kiwanda hicho kinachotengeneza mvinyo aina ya Raha ,kinatumia mfumo wa kisasa wa kudhibiti  Maji taka yanayotoka kiwandani ili kuweza kutumika Kwa matumizi mengine bila kuleta madhara.

 

Alisema Kampuni ya Raha Bereveges wa muda mrefu imekuwa ikitumia mfumo huo wa kisasa wa kusafisha Maji taka ya kiwandani ili kuweza kutumika Kwa ajili ya umwagiliaji wa mimea bila kuwa na madhara .

 

 

“Maji yetu yanapimwa na watu wa Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka Arusha,(AUWSA) na Baraza la Taifa la Uhifadhi na Usimamizi wa Mazingira, (NEMC) na wamethibitisha maji yetu ni salama hayana madhara kwa mwanadamu na yanaweza kutumika kwenye umwagiliaji wa mime,” amesisitiza Olomi na kuongeza.

 

 

“Sisi tunazalisha mvinyo , raha poa na raha gold utokanao na ndizi na malighafi tunanunua hapahapa nchini ikiwemo ndizi, sukari, hamira na tunaajiri wananchi hivyo mbali ya kulipa kodi lakini tunachangia kutoa ajira zaidi,”.

 

Meneja rasilimali watu wa kampuni ya Raha Beverages limited, Beatha Antony.

 


“ Tunawaomba Watanzania nao watusapoti kwa kutumia vinywaji vyetu vyenye ubora wa hali ya juu uliothibitishwa na Shirika la viwango nchini, (TBS)na vina stamp ya kodi hivyo wanywaji wetu waangalie kwenye kizibo kuona kama zina stika hizo,” amesema Meneja rasilimali watu wa kampuni hiyo, (human resource) Beatha Antony.

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

0 Comments:

Post a Comment