Mazishi ya aliyekuwa Mkuu wa Polisi Wilaya ya Kipolisi Chanika, SP Awadh Mohamed Chico, yamefanyika leo, Machi 18, 2025, baada ya kifo chake kilichotokea katika ajali ya gari jana akiwa anaelekea kazini.
Naibu Kamishina wa Jeshi la Polisi (DCP) Mkondya ameongoza waombolezaji katika ibada ya kuaga mwili wa marehemu, ambapo alitoa salamu za rambirambi kwa familia ya SP Awadh kwa niaba ya Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini (IGP), Camillus Wambura.
Aliwahimiza waombolezaji kuwa wavumilivu katika kipindi hiki kigumu, akisema kuwa safari ya umauti ni ya kila mmoja wetu.
Ajali hiyo ilitokea maeneo ya Gongolamboto mwisho, karibu na Kilima cha kuingia Pugu Sekondari, ambapo SP Awadh Mohamed Chico alipoteza maisha baada ya gari lake aina ya Prado kugongana na basi aina ya Eicher.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala, ACP Yustino Mgonja, alithibitisha kifo cha SP Awadh kupitia mitandao rasmi ya kijamii za Jeshi la Polisi.
Bofya kusoma zaidi
Kifo cha SP Chiko Kufuatia Ajali ya Gari: Maziko Kufanyika Kesho Kijitonyama
0 Comments:
Post a Comment