WAZIRI Mkuu Kassim Majaliwa amesema kuna matumizi mabaya fedha za UVIKO 19 zilizopelekwa kwenye Bohari ya Dawa ya Taifa, (MSD) hivyo ameiagiza Bodi ya Wataalamu ya Ununuzi na Ugavi (PSPTB) kuwachukulia hatua haraka waliohusika.
Aidha ameahidi
kutembelea MSD Jumatatu Mei 9 mwaka huu akiambatana na Mkuu wa Jeshi la Polisi
nchini na Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) kupata
maelezo ya kina juu ya wizi huo.
Waziri Mkuu ameyasema
hayo leo (Alhamisi, Mei 5, 2022) wakati akizungumza na wataalamu wa ununuzi na
ugavi pamoja na wasimamizi kwenye uzinduzi wa wiki ya Ununuzi wa Umma iliyoanza
leo jijini Arusha.
Alisema kitendo
kilichofanywa na wasimamizi wa ununuzi wa umma ambao wanaaminiwa na serikali kukubali
zabuni za watoa huduma zenye bei ya juu kuliko bei halisi za soko hakivumiliki na
kuahidi kuwa ataanza na MSD kulishughulikia suala hilo.
"Pamoja na uwepo wa
taasisi zinazosimamia manunuzi yanayofanywa katika ofisi zetu, bado wasimamizi
wa manunuzi hawajaona huruma kwa walioa kodi wetu kwa kuendelea kufanya
manunuzi kwa gharama kubwa," alisema Waziri Mkuu.
Akitoa mfano alisema MSD
walitakiwa kununua kipimo cha sukari, (blood glucose test) ambacho kwa bei ya
kawaida ni Sh.150 ila wao wakanunua kwa Sh. 300, kipimo cha mkojo (urinalysis)
bei ya kawaida Sh. 200 kimoja wao wakanunua kwa Sh. 780.
"Walitakiwa kununua
kipimo kidogo cha hematolojia ya mwili, (full blood picture 3 part) kinauzwa
Sh. 2,100 wao wanaonyesha wamenunua kwa bei ya zabuni Sh 4,500.
“Lakini pia walipaswa
kununua kipimo kikubwa cha Haemolojia ya mwili bei ya kawaida ni Sh. 3,800 wao
wamenunua kwa sh. 6,300,si mnaona hizi bei zinavyokwenda watu hawana
huruma na watanzania wenzao,"alisema Majaliwa
Aidha aliwndelea kutoa
mfano wa upigaji huo kuwa kipimo cha kuangalia ufanyaji kazi wa figo
ambacho kipimo muhimu sana na vingepatikana kwa wingi kinachouzwa
Sh.6,000 wao wamenunua kwa Sh 40,000.
Pia,alisema walitakiwa
kununua seti moja ya vitendanishi kwa ajili ya awamu moja ya kusafisha damu bei
ya kawaida ambayo wangepaswa kununua ni Sh. 65,000 lakini wao wamenunua kwa Sh.
189,000
Majaliwa alisema MSD
walitakiwa wanunue mashine ndogo ya kipimo cha haimolojia ya mwili ambacho
kinauzwa Sh.milioni tano wao wamenunua kwa Sh. milioni 14.045,huku wakitakiwa
kununua mshine ndogo ya kupima kemia ya mwili ambayo bei ya kawaida ni
Sh.milioni 1.35 ila wao wamenunua kwa bei ya Sh. milioni 6.7.
“Nyingine walitakiwa
kununua mashine kubwa ya kupimia kemia ya mwili ambayo bei ya kawaida ni
Sh.milioni 10.5 wao wamenunua kwa Sh.milioni 49.hawa walitakiwa wanunue mashine
ya kupima sukari kifaa hiki kinauzwa Sh. 7.956 wao wamenunua kwa Sh. 58,500.
“Hawa walitakiwa kununua
mashine kubwa ya kupimia haimolojia ya mwili hiki kifaa kinauzwa Sh. milioni
20.8 lakini wamenunua Sh milioni 117,hawa pia walitakiwa wanuue kifaa kinaitwa
mashine ya kupimia haimolojia ya mwili cha ukubwa kidogo bei ya kawaida ni Sh.
milioni 37.4 wao wamenunua Sh.milioni 149.4.
"Hebu wataalamu
wetu mtuambie ni kwa sababu ya nini,wataalamu wetu wa manunuzi kwa nini hili
linatokea?kwa maslahi ya nani“Je tukichukua hatua tena kali,vyombo vyote mko
hapa vya manunuzi haya ndiyo yanayoendelea kwenye ofisi zetu,kwa wale wachache
wasio kuwa na nia njema na fedha za walipa kodi wa nchi hii,"alisema
Alisema ongezeko hilo la fedha zilizopotea kwa ujanja wa watu wasiozingatia sheria,taratibu, kanuni za ununuzi wa umma ambazo zingenunua vifaa kwa wingi, lakini wamenunua kifaa kimoja tu huku watanzania wanasubiri kupata vifaa vingi visambae kwenye hospitali,zahanati na vituo vya afya
Aidha alisema mtu mmoja
anakwamisha watanzania kupata huduma walizotahili na ni watu walioaminiwa
ba serikali kusimamia fedha za umma.
"Jumatatu nikukute
pale saa nne asubuhi wanipe maelezo haya na mimi sitasita kwenda na
Kamanda Siroo na Hamhuduni ili washughulike na ha o na tunapoanza na hao huwa
hawabaki kazini,hii sio nia ya serikali yenu ila mnatulazimisha,"alisema.
Naibu wa Fedha na
Mipango, Hamad Chande alisema serikali imeboresha na kuondoa vifungu
vilivyokuwa na vikwazo katika ununuzi wa umma.
Ofisa Mtendaji Mkuu wa
Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa umma (PPRA) Irene Isaka,alisema wiki
hiyo ya ununuzi wa umma inakauli mbiu ya "Matumizi ya Teknolojia latika
kuboresha ununuzi wa umma" na inawashiriki 1003.
Waandaaji wa mkutano huo
ni Mamlaka ya Kudhibiti Ununuzi wa Umma (PPRA), Wakala wa Huduma za Ununuzi
Serikalini (GPSA), Mamlaka ya Rufaa za Zabuni za Umma (PPAA) na Bodi ya
Wataalamu wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB) na unahudhuriwa na wadau mbalimbali wa
ununuzi nchini wakiwemo madiwani.

0 Comments:
Post a Comment