TUME ya Taifa ya Uchaguzi imesema kuwa imeanza mchakato
wa kuboresha daftari la wapiga kura ili liweze kutumiaka kwenye upigaji kura ya
maoni ya katiba mpya.
Aidha, zoezi hilo
linatarajiwa kutumia zaidi ya sh 279 bilioni mpaka kukamilika ingawa haijajulikana
zoezi hilo litatumia muda gani kukamilika.
Hayo yalisemwa leo jijini hapa na Mwenyekiti wa Tume ya
Uchaguzi, (NEC), Jaji Damian Lubuva alipokuwa akiongea na viongozi wa vyama vya
siasa vinavyoshiriki uchaguzi mdogo wa Udiwani Kata ya Sombetini pamoja na
waandishi wa habari.
0 Comments:
Post a Comment