Monday, May 26, 2025

Rais Dkt. Samia Ateua Viongozi Wapya wa NCAA na PSSSF




Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amefanya mabadiliko ya uongozi kwa kuteua viongozi wapya katika Mamlaka ya Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro (NCAA) na Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF).

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo, Mei 26, 2025, na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Dkt. Moses Kusiluka, uteuzi huo ni kama ifuatavyo:



“Abdul-Razak Badru ameteuliwa kuwa Kamishna wa Uhifadhi wa Mamlaka ya Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro (NCAA),” imeeleza taarifa hiyo.
Kabla ya uteuzi huu, Abdul-Razak Badru alikuwa Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF). 


Anachukua nafasi ya Elirehema Joshua Doriye, ambaye uteuzi wake umetenguliwa.

Wakati huo huo, “Himo Simeon Nyansaho ameteuliwa kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF),” imeongeza taarifa hiyo.

Kabla ya uteuzi huu, Himo Nyansaho alikuwa Mkurugenzi wa Maendeleo ya Biashara katika Benki ya Azania.

Taarifa hiyo imetolewa na Sharifa Nyanga, Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu, Dodoma.

No comments:

Post a Comment