Friday, April 1, 2022

WALIMU WAWILI WA SAYANSI WAFUNDISHA ZAIDI YA WANAFUNZI 1,000 KITETO


Mohamed

KUTOKANA  na uhaba wa waalimu wa masomo ya Sayansi, wanafunzi zaidi ya 1,069 wa shule ya Sekondari Kiteto iliyopo Mkoani Manyara wanafundishwa na walimu wawili waliopo.

 Mwenyekiti wa Halmashauri ya Kiteto, Abdalah Bundaka(Bwangadimwe) akiungumza na wanafunzi wa Kiteto Sekondari wazazi na walezi kwenye maafali ya kidato cha sita 2022.kulia ni John Kimaro Mkuu wa shule hiyo Picha na Mohamed Hamad.


Mkuu wa shule ya Sekondari Kiteto, John Kimaro, akizungungumza mbele ya Mwenyekiti wa halmashauri ya Kiteto kwenye maafali ya kidato cha sita (jana) alisema idadi ya wanafunzi Kiteto Sekondari haiendani na ikama ya walimu waliopo.


"Mhe. Mwenyekiti hapa tuna walimu 37 tu, na tuna zaidi ya wanafunzi 1,000 kuanzia kidato cha kwanza hadi cha sita tunachangamoto kubwa ya ufundishaji kwa uwezo wako tunaomba msaada wa kupayiwa walimu"


Kwa kuwa wewe unayo nafasi ya kuonana na viongozi mbalimbali tufikishie kilio chetu huko..tunaomba utuondolee hii adha kwani hawa wanafunzi wanaendelea kukosa masomo


Haki ya elimu kwa mwanafunzi iko kikatiba kwani huwezi amini hapa tuna waalimu wawili tu wa masomo ya Sayansi tunapaswa kuwa na zaidi ya hao ili tutoe huduma lakini unawezaje kuingia madarasa yote walimu wawili.


Akizungumzia uhaba wa waalimu Abdalah Bundala mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Kiteto mbele ya wanafunzi waalimu na wazazi aliwaahidi kuwa atashughulikia tatizo hilo kwani mpaka sasa pamoja na uhaba wa waalimu hao shule hiyo imekuwa ikifanya vizuri


Nao baadhi ya wanafunzi akiwemo James Elieta kidato cha Sita alisema, pamoja na uhaba wa waalimu unachochea utoro kushuka kiwango cha elimu pamoja na wanafunzi kutofikia ndoto zao kikamilifu zipo jitihada kubwa ambapo mwaka jana walipata ufaulu wa div 1 poiti saba.


Alisema awali wazazi walilazimika kutumia gharama kubwa kuwatafutia watoto wao shule nje ya wilaya na maeneo mengine ya Kiteto hivyo kupatikana shule hiyo kumepunguza gharama kwa wazazi pamoja na kuongeza idadi ya wasomi nchini.


 

No comments:

Post a Comment