SEKTA
ya utalii nchini imeanza kuinuka baada ya kukumbwa na athari zitokanazo na
ugonjwa wa UVIKO 19 ambapo kwa mwaka 2021 kumekuwa na ongezeko la asilimia 48.6
la watalii wa kimataifa waliotembelea nchini huku mapato yatokanayo na sekta ya
utalii yakiongezeka kwa asilimia 76.
Hayo yasemwa Machi 28,2022 jijini Arusha na Katibu Mkuu wizara ya
Maliasili na Utalii, Dkt Francis Michael wakati akizindua mafunzo ya upangaji wa
madaraja wa na upimaji ubora wa huduma
za malazi na chakula Chuo cha Taifa Cha Utalii, (NCT) kampasi ya Arusha.
Katika hotuba yake iliyosomwa kwa niaba yake na Mkurugenzi wa Utalii, Wizara ya Maliasili na Utalii, Philip Chitaunga, Dkt. Francis amesema kuwa baada ya dunia kukumbwa na janga la UVIKO 19 idadi ya watalii wanaofika nchini ilishuka kwa asilimia 59.3 na mapato yalishuka kwa asilimia 72.5.
“Lakini
janga na UVIKO 19 limeiathiri sekta hii kama ilivyotokea kwenye nchi nyingine
duniani kote, lilisababisha watu wasisafiri kwani utalii unahusisha kusafiri
sasa watu waliacha kusafiri, ndege zikaacha baadhi ya safari zake kila kitu
kilisimama,” amesema Dkt,Francis na kuongeza.
…Sisi
kama nchi masoko yetu ya utalii nayo yaliathirika kwani watu walikuwa hawaji Tanzania na
biashara zetu zilianguka, hoteli nyingi zilifungwa biashara za utalii
ziliathirika idadi ya watalii ilishuka kwa asilimia 59.3 na mapato yalishuka
kwa asilimia 72.5. hii ni anguko kubwa sana,”.
Hata
hivyo amesema Serikali kwa kushirikiana
na na sekta binafsi walichukua hatua mbalimbali kuhakikisha wanarejesha sekta
ya utalii katika hali yake ya kawaida miongoni mwa mambo yaliyofanyika ni
kuandaa muongozo ulioiongoza sekta ya utalii kufanya shughuli zake wakati wa
janga la UVIKO 19.
“Tuliandaa
‘Standard Oparating Procedure’, tuliandaa mpango wa kurejesha utalii katika
hali yake ya kawaida, tuliandaa mafunzo kwa wale ‘front liners’ wote kwenye hii
sekta,” amesema Katibu mkuu huyo akieleza namna walivyofanikiwa kuongeza idadi
ya watalii nchini na kuongeza
…Hii
ilitusaidia sana, shirika la kimataifa linalosimamia utalii na usafiri ‘World Tourism
and Travel council’ liliipatia Tanzania ‘safe travel stamp’ kueleza kuwa Tanzania ni sehemu salama ambayo
watu wanaweza kusafiri.
…Hii
iliwezesha watalii kujenga imani na sisi hivyo hata wakati wa UVIKO 19 watalii
waliendelea kutembelea Tanzania ambapo
mwaka 2021 tumekuwa na ongezeko la asilimia 48.6 la watalii wa kimataifa
waliotutembelea nchini,”
Dkt
Francis amesema hapa nchini kwenye mpango wa utoaji chanjo ya UVIKO 19 sekta ya utalii imekuwa miongoni mwa sekta
zilizopewa kipaumbele ndiyo sababu wamepatiwa fedha za kutoa mafunzo hayo yatakayosaidia
kuboresha viwango vya huduma za sekta ya utalii hivyo kuifanya Tanzania kuwa
miongoni mwa nchi shindani katika kuboresha huduma na hivyo kujenga imani kwa
wageni wanaokuja nchini.
“
Mpango wa maendeleo na ustawi wa Taifa na mapambano dhidi ya UVIKO 19 tumepata
fedha hizi zinazotumika kutoa mafunzo haya yatakayosaidia kuboresha utendaji wa
sekta hiyo na kufikia malengo ya kupokea watalii milioni 5 ifikapo mwaka 2025
kama ilani ya chama tawala, (CCM) inavyoeleza,” amesisitiza Katibu Mkuu huyo wa
Wizara ya Maliasili na Utalii.
Amesema
sekta vya utalii ina mchango mkubwa sana katika uchumi wa nchi wa nchi kwani kabla
ya janga la Uviko 19 mwaka 2019 sekta hiyo ilikuwa ikichangia asilimia 17 ya
pato la Taifa sawa na dola za Marekani bilioni 4.2 kwenye pato la Taifa na imekuwa ikichangia asilimia 25 ya mauzo yote ya
nje yanayohusu huduma.
“Lakini
pia imekuwa ikitoa ajira za moja kwa moja na zisizo za moja kwa moja milioni
1.6 kama ambavyo mnafahamu sekta ya utalii huwa inachochea maendeleo ya sekta
nyingine. Sehemu ambayo utalii umekua na shughuli nyingine za kibiashara zimekua,”
amesisitiza Dkt. Francis na kuongeza.
Sekta
ya utalii imekuwa muhimu katika kukuza uchumi, kutoa ajira na maendeleo mengine
kwa mtu mmoja mmoja na Taifa kwa ujumla.
Akizungumzia
juu ya mafunzo hayo yanayotolewa kwa washiriki 44, Katibu Mkuu huyo wa Wizara
ya Maliasili na Utalii amesema kuwa ameambiwa mtaala utakaotumika ni ule uliopitishwa
na Jumuiya ya Afrika Mashariki, (EAC) hivyo wasahihishaji wa mitihani si lazima wawe
wakufunzi waliowafundisha hapo bali wanaweza kutoka kwenye nchi yoyote mwanachama.
“Hii
siyo semina hii ni shule tunatarajia mnasoma ili mfaulu itakuwa ni aibu sana kwamba
umekaa hapa miezi miwili halafu unatoka hapa unarudi nyumbani umefeli. Si kitu ambacho sisi tunakitarajia,”
amesema Chitaunga akisoma hotuba hiyo ya Katibu Mkuu wa wizara ya Maliasili na
utalii na kuongeza.
…Tupambane
tuhakikishe yale wakufunzi wetu watatupatia tutayaweka vizuri kichwa mwetu
tuweze kuhakikisha kwamba sisi wote 44 tulioanza mafunzo haya tumefauli.
…Mafunzo
haya pamoja na kulenga katika ukarimu lakini pia yatahusisha maeneo mengine ya
utoaji huduma kama vile ubora wa mazingira , usalama mahali pa kazi, masuala ya
ajira, bima, ulinzi na usalama.
…Ninawasihi
Chuo Cha Taifa Cha Utalii ambao ndiyo wanatoa mafunzo husika na wadau wengine watakaohusika
kutoa mafunzo hayo kuhakikisha wanatoa maelezo muhimu kwa washiriki ili waweze
kuelewa umuhimu wa kila jambo katika yale wanayofundishwa.
Awali, Mkurugenzi wa NCT, Dkt, Shogo Mlozi
ameishukuru EAC, Sekretarieti ya Uzalishaji na
Jamii kwa kuwezesha kitengo chake cha usimamizi wa upangaji wa madaraja na
upimaji ubora wa malazi na chakula kwa kuweza kuratibu mafunzo hayo kwa
kushirikiana na NTC.
Amesema NTC inatoa mafunzo ngazi ya
cheti na diploma ambapo wana matawi manne nchini likiwemo hilo la Arusha,
Mwanza na mawili jijini Dar es Salaam.
“NTC kwa sasa imepewa jukumu la
kuendesha mafunzo ya aina mbili kupitia
mpango wa maendeleo kwa ustawi wa Taifa na makabiliano ya UVIKO 19 na Wizara
yako unayoisimamia,” amesema Dkt Mlozi na kuongeza.
…Kama chuo tumeshamaliza mafunzo ya
awamu ya kwanza tuliyopewa ambayo ilikuwa ni mafunzo ya kuwaongezea ujuzi wadau
muhimu katika mnyororo wa Utalii katika mikoa nane Tanzania Bara ambapo jumla
ya washiriki 1,200 wamenufaika na mafunzo hayo,”.
Mkurugenzi huyo wa NCT amesema
washiriki hao walitokea mikoa ya Lindi, Mtwara, Ruvuma, Njombe, Iringa, Mbeya,
Mara na Mwanza ambapo mafunzo hayo yalitolewa kwa watu kati ya 100 na 150 kwa kila
mkoa kulingana na ukubwa wa eneo.
Dkt Mlozi amesema kuwa mafunzo ya
sasa ni awamu ya pili ambayo ni ya
upangaji madaraja na upimaji wa ubora wa huduma za chakula na malazi yanatolewa
kwa washiriki 44 kati yao 14 wanatoka kwenye sekta binafsi na 30 kutoka sekta
ya umma.
“Mafunzo haya yanaenda kutolewa na
wataalam wanaotambulika na EAC ambayo kwa hapa nchini ni wachache sana wako
mama Salama Kibogoyo, Joseph Ntimba, Franline Mwinyimbegu, Kemirabi Kibogoro na
Burhan Hassan,” amesema Dkt Mlozi na kuongeza.
“Aidha mafunzo hayo yataambatana na
mafunzo ya wakufunzi wa wataalam saba ambao walishiriki mafunzo ya wataalam wa upangaji
wa huduma za malazi katika ubora mwaka 2011 ambapo mafunzo yao yatakiwa ya wiki
nne,”.
Dkt Mlozi amesema taratibu za utoaji
huduma za chakula na malazi wakati huu wa janga la UVIKO 19 zimebadilika ambapo
mabadiliko haya yanatakiwa kuzingatiwa katika upangaji wa madaraja na upimaji
wa ubora wa chakula na malazi hivyo kufanya mafunzo haya kuwa ni ya muhimu sana
kutolewa nyakati hizi ambazo kama nchi na dunia tunaendelea kukabiliana na
janga hili la UVIKO 19.
“Mafunzo haya yamelenga kuandaa
wataalam ambao wataenda kutoa weledi kwa watoa huduma juu ya namna mpya ya
kuendesha biashara ya utalii na kusaidia kuinua viwango vya ubora katika sekta
ya utalii nchini,” amesema Dkt Mlozi na kuongeza.
…Hii itasaidia kuonyesha Tanzania
imejiandaa vema katika kuhakikisha wageni wa ndani na wa nje wanapata huduma zenye
ubora kama inavyotarajiwa na kamba ambavyo Tanzania imewekwa kwenye ramani ya
dunia kama sehemu salama ya kutembelea,”.
Kwa upande wake, Katibu Tawala mkoani Arusha, (RAS), Dkt Athuman
Kihamia aliyewakilishwa na Afisa elimu mkoani hapa, Abel Ntupwa aliwahimiza
washiriki hao mara watakapohitimu wakatekeleze majukumu yao kwa kuzingatia
maadili ikiwemo kutunza siri na kuepuka vitendo vya rushwa.
Naye
Afisa anayeshughulikia Masuala ya Utalii kutoka Sekretarieti ya EAC, Dkt. Simon Kiarie ameipongeza Tanzania kwa
kuwa mstari wa mbele katika kutekeleza mapendekezo yaliyotolewa na jumuiya hiyo
katika kukabiliana na athari za UVIKO 19 kwenye sekta ya utalii.
Akiongea
kwenye mkutano huo kwa njia ya mtandao amesema kuwa UVIKO 19 ulisababisha idadi
ya watalii wanaotembelea ukanda huu kushuka kwa asilimia 70 kutoka watalii
milioni 7 mpaka watalii milioni 2.26 kwa mwaka.
Kiarie
amesema nchi wanachama wanapaswa kufanya juhudi za pamoja kuhakikisha wanarudi
kwenye idadi ya awali ya wastani wa watalii milioni 7 waliokuwa wakitembelea
vivutio vilivyo kwenye ukanda huu.
Amesem
kuwa EAC iliweka mipango kadhaa ya kuinua utalii ikiwemo kuanzisha maonyesho ya
utalii ambapo aliipongeza Tanzania kwa kuyafanya jijini Arusha mwaka jana.
Kiarie
amesema kuwa Tanzania imekuwa nchi ya kwanza kwenye nchi zinazonda EAC kutoa mafunzo hayo ya usimamizi wa upangaji wa madaraja na upimaji ubora wa malazi
na chakula Suala
la ubora wa huduma na chakula ni mambo ambayo ni miongoni mwa masuala
yaliyoazimiwa na EAC.



No comments:
Post a Comment