RUFAA ya aliyekuwa
Mkuu wa wilaya Hai, Lengai Ole Sabaya na wenzake wawili imepangiwa
kusikilizwa kwenye Mahakama Kuu Kanda ya Arusha, mbele ya jaji, Butamo Philip kuanzia
desemba 13, mwaka huu.
Wakili, Edmund Ngemela
anayemwakilisha mrufani wa pili, Silvester Nyegu aliwaeleza waandishi wa habari leo Novemba 16,2021 kuwa siku hiyo
shauri hilo litafika mahakamani hapo kwa ajili ya kutajwa.
Rufaa hiyo iliyosajiliwa namba 129/2021 inatokana na kesi ya jinai namba 105/2021 ambayo ilisikilizwa kwenye mahakama ya hakimu mkazi Arusha na hakimu mkazi Mwandamizi, Odira Amworo ambapo Oktoba 15, mwaka huu walihukumiwa kifungo cha miaka 90 jela kwenye makosa matatu waliyokutwa na hatia.
Kifungo hicho ni adhabu
ya miaka 30 jela kwa kila kosa walilokutwa na hatia ambapo kila mmoja alikutwa
na hatia kwenye makosa matatu tofauti ya unyang'anyi wa kutumia nguvu na
unyang'anyi wa kutumia silaha.
Hata hivyo mahakama
iliamua adhabu hizo ziende kwa pamoja hivyo kila mmoja atatumia kifungo
cha miaka 30 jela.
Hata hivyo wakili Ngemela alisema kuwa wanasababu za rufaa zaidi ya 10 ingawa hakutaka kuingia kwa undani
juu ya kile lilichopo ndani ya rufaa hiyo.
HUKUMU ILIKATIWA RUFAA
Awali hukumu hiyo ilitolewa na Hakimu Mkazi Mwandamizi Odira Amworo, Oktoba 15,2021 majira ya saa 11:47 jioni baada ya kuanza kusoma hukumu hiyo
kuanzia majira ya saa 5:56 asubuhi.
“Kama alivyosema wakili wa serikali mwandamizi, Felix Kwetukia
kwamba mshitakiwa wa kwanza Lengai Ole Sabaya alikuwa mkuu wa wilaya
aliyeteuliwa na Rais kitendo alichofanya kinadhalilisha taasisi ya Rais,”
amesema Hakimu huyo na kuongeza.
…Na hakuna ubishi kwamba wote ni vijana na wanahitajika kama
walivyoeleza mawakili wao na kwa mujibu wa sheria hakuna ubishi kwamba mikono
yangu imefungwa naweza kuwafunga miaka 100 lakini kurudi chini siruhusiwi
kufunga chini ya 30...
…Mbali ya kwamba wakili wa serikali ameomba viboko wachapwe na
walistahili wachapwe manake nao walikuwa wanawatoa wenzao wenge…
(Mahakama kicheko)
…Lakini mawakili wenzetu wameshindwa kuinyambulisha sheria ya
zamani ya watoto walikuwa wanapigwa viboko lakini sheria mpya hawapigwi viboko
wamepenyea hapo angalau. Basi mikono yangu imefungwa adhabu ya chini
miaka 30 na viboko…
…Kosa la kwanza kila mshitakiwa miaka 30 kila mmoja kosa la pili
miaka 30 kila mmoja na kosa la tatu miaka 30 kwa kila mmoja, kwa viboko
mawakili wameshinda sitatoa viboko na adhabu ziende pamoja.Mna haki ya rufaa
iko wazi,”.
No comments:
Post a Comment