Saturday, January 23, 2021

CORONA YATAJWA KIFO CHA LARRY KING

 


Mtangazaji maarufu nchini Marekani Larry King amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 87 huko Los Angeles.


King ameaga dunia Jumamosi katika kituo cha matibabu cha Cedars-Sinai kulingana na Ora Media, kampuni ambayo yeye pia ni mshikiri wa uanzilishi wake.

Wakati wa taaluma yake ya miaka 60, ambayo ni pamoja na miaka 25 ya kuwa mtangazaji wa kipindi chake mwenyewe katika Shirika la CNN, King alihoji viongozi wengi maarufu wakiwemo wanasiasa, wasanii na hata wanamichezo.

Mwezi huu, alitibiwa ugonjwa wa virusi vya corona, vyombo vya habari vya Marekani vimesema.

No comments:

Post a Comment