Sunday, January 31, 2021

BABA AMCHOMA MTOTO WAKE


 Kamanda wa polisi mkoani Arusha, (RPC), Salumu Hamduni

MKAZI wa Elerai jijini Arusha, Badru Abdallah, (38) anadaiwa kumchoma kwa pasi mtoto wake mwenye umri wa miaka 12.


Kamanda wa polisi mkoani hapa, Salumu Hamduni ameeleleza kupitia taarifa yake aliyoitoa jana kwa vyombo vya habari kuwa tukio hilo lilitokea januari 16, mwaka huu majira ya saa mbili usiku.

Mtoto mdogo jina limehifadhiwa miaka 12, alijeruhiwa kwa kuchomwa na pasi ya umeme mgongoni na Baba yake mzazi aitwaye Badru Abdallah, (38), )mrangi na mkazi wa Elerai," alisema kamanda Hamduni.


Alisema kuwa  mtuhumiwa anashikiliwa na Jeshi la Polisi na mara baada ya upelelezi kukamilika jalada litapelekwa ofisi ya Taifa ya mashtaka kwa ajili ya hatua zaidi. 


No comments:

Post a Comment