Thursday, January 21, 2021

AMRI ALIZOSAINI BIDEN

Rais Biden akisaini haraka amri za rais juu ya virusi vya corona, mabadiliko ya tabia nchi na ukosefu wa usawa
Rais Biden "atachukua hatua - na si kubadili sera peke yake ya uharibifu uliofanywa na utawala wa Trump- lakini pia kuanza kuliendeleza taifa," taarifa inayofafanua amri hiyo inaeleza.

Mfululizo wa hatua zitakazotekelezwa kukabiliana na janga la virusi vya corona ambalo limesababisha zaidi ya vifo 400,000 nchini Marekani.

Bwana Biden anataka Wamarekani milioni 100 kupewa chanjo ndani ya siku 100 za mwanzo wa madaraka yake.

Kutakuwa na amri ya uvaaji wa barakoa na kukaa kwa umbali katiika maeneo yote ya umma.

Ofisi mpya itaweka mkakati wa kukabiliana na janga hilo la corona - na kuanzia na hatua ya utawala wa Trump - kuiondoa Marekani katika Shirika la Afya (WHO).

Bomba lililofadhiliwa kibinafsi - linalokadiriwa kugharimu karibu dola bilioni 8, itakayobeba malighafi za mafuta kutoka Alberta, nchini Canada, mpaka Nebraska.

Barack Obama alipiga kura ya kuidhinisha muswada wa ujenzi wa bomba mnamo 2015 lakini uamuzi huo ulibatilishwa na Rais Trump.

Kuhusu uhamiaji Bw Biden amebatilisha tangazo la dharura la utawala wa Trump ambalo lilisaidia kufadhili ujenzi wa ukuta kando ya mpaka wa Mexico na pia kumaliza marufuku ya kusafiri kwa nchi nyingi za Waislamu.
Amri zingine zinahusu usawa wa kijinsia.

No comments:

Post a Comment