Thursday, August 24, 2017

TANGAZO: TANGAZO LA MKOPO KWA WANAWAKE WA JIJI LA ARUSHA

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
OFISI YA RAIS
TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA

 

Anwani ya Simu “REGCOM”                                                                 OFISI YA MKUU WA MKOA,
Simu: 2545608/2545820/2545872                                                                                  P.O. BOX 3050,
Fax: 2545239/2544386                                                                                                           21 /08/2017                                                                                               ARUSHA.


TANGAZO LA MKOPO KWA WANAWAKE WA JIJI LA ARUSHA
1.0  Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Arusha kupitia fedha za marejesho ya pikipiki za UBOJA (Revolving funds) anawatangazia wanawake wa Jiji la Arusha kuwa anatarajia kuwawezesha wanawake 500 ambao ni wafanyabiashara wadogowadogo au wanaotegemea kuanza biashara ndogondogo kwa ajili ya kujikimu kimaisha kwa kuwapatia  kiasi cha Tsh 200,000/=kama mkopo usiokuwa na riba na masharti magumu. Mkopo huu utalenga mwanamke mmoja moja/ kundi la wanawake watakao timiza vigezo.
    2.0     VIGEZO VYA KUPATA MKOPO
                 I.   Awe/Wawe wanawake wenye kipato cha chini, kundi la wanawake waliopo kwenye Biashara ndogondogo.
               II.   Wawe wenye mawazo ya kufanya Biashara na hawana mtaji wa kuanzisha biashara zao.
             III.   Kipaumbele cha mkopo huu ni kwa wanawake wajane na yatima.
             IV.   Wawe wakazi wa Kata husika na Mtaa husika ndani ya Jiji la Arusha, awe anafahamika/anatambulika kwa viongozi wake wa mtaa yaani Mtendaji wa mtaa.
               V.   Asiwe na mkopo kutoka mahali pengine ili kurahisisha marejesho yake ya kila wiki.
             VI.   Awe na wadhamini wawili (2) wanaofahamika ndani ya Mtaa na Kata husika

3.0      Wanawake wote watakao kidhi vigezo tajwa hapo juu mnakaribishwa kuwasilisha maombi yenu ya mkopo katika Ofisi ya Kata unayoishi, maombi hayo yaambatanishwe  na utambulisho wa Mtendaji wa mtaa  unaoishi.

 4.0       Mwisho wa kuwasilisha maombi ni siku kumi na nne(14) kuanzia tarehe ya tangazo hili tarehe 21/o8/2017 hadi tarehe 4/9/2017, na bahasha za maombi zitafunguliwa mbele ya waombaji watakao penda kuhudhuria.

5.0       Taarifa za matokeo ya waliofanikiwa kupata mkopo zitatolewa kupitia Ofisi za Kata baada ya uchambuzi wa kina kufanyika kwa kuzingatia vigezo vilivyo ainishwa.
6.0       wanawake watakao fanikiwa kukidhi vigezo vya mkopo watapewa mafunzo ya ujasiriamali bure kabla ya kupewa mkopo.

7.0        NAMNA YA KUREJESHA MKOPO
                 I.   Marejesho yatafanyika kwa  kipindi cha miezi mine (4) ukiwepo mwezi mmoja  (1) wa Matazamio hivyo muda wa kukamilisha marejesho utakuwa ni kipindi cha miezi mitano (5)
               II.   Fedha zote  za marejesho zitapelekwa Benki kwenye akaunti maalumu itakayofunguliwa kwa ajili ya marejesho ya mikopo hiyo.

Mnakaribishwa kwa maombi.

Imetolewa na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa

No comments:

Post a Comment