Akizungumza ofisini kwake mapema hii leo asubuhi, Lema amesisitiza kuwa huu ni uvunjifu wa Amani. Kwani sheria za nchi zinamruhusu mtu yeyote kufanya mkutano popote ilimradi iwe ndani ya mpaka ya nchi.
"Esther Bulaya amewekwa ndani kwa kosa ambalo hata kwenye katiba ya nchi hii halipo"
" mbunge wa bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania anaruhusiwa kufanya mkutano mahala popote nchini ."Alisema Lema.
Lema amesema Jeshi la polisi halipaswi kutekeleza kila amri wanayopatiwa na wakuu wa wilaya badala yakwe linapaswa kufanya kazi zao kwa weledi wakizingatia katiba na sheria za nchi katika kutekeleza majukumu yao ya kulinda usalama wa raia na mali zao.
Lema Amelaani vikali nakuonesha masikitiko yake kufuatia kukamatwa kwa Mbunge wa Bunda, Esther Bulaya kwa kile alichodai kuwa ni kwa maelekezo ya mkuu wa wilaya.
Alidai wameambiwa Bulaya wanashikiliwa kwa tuhuma za kufanya mkutano wa hadharani kwenye jimbo Tarime Vijijini.
Katika hatua nyingine Mbunge Lema amewataka viongozi wa Tanzania kuiga kwa Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta ambaye ameruhusu maandamano ya kumpinga.
"Rais Uhuru Kenyatta amewapa amri askari polisi Kuwalinda waandamanaji waliotaka kuandamana kupinga ushindi wake huu ni mfano wa kuigwa hasa ikizingatiwa hili linatokea katika nchi za Afrika Mashariki,".
Lema amewaomba viongozi wa dini kukemea kile alichodai kuwa ni udhalilishaji wa viongozi , pamoja na uvunjifu wa sheria za nchi .
"Esther Bulaya amewekwa ndani kwa kosa ambalo hata kwenye katiba ya nchi hii halipo"
" mbunge wa bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania anaruhusiwa kufanya mkutano mahala popote nchini ."Alisema Lema.
Lema amesema Jeshi la polisi halipaswi kutekeleza kila amri wanayopatiwa na wakuu wa wilaya badala yakwe linapaswa kufanya kazi zao kwa weledi wakizingatia katiba na sheria za nchi katika kutekeleza majukumu yao ya kulinda usalama wa raia na mali zao.
Lema Amelaani vikali nakuonesha masikitiko yake kufuatia kukamatwa kwa Mbunge wa Bunda, Esther Bulaya kwa kile alichodai kuwa ni kwa maelekezo ya mkuu wa wilaya.
Alidai wameambiwa Bulaya wanashikiliwa kwa tuhuma za kufanya mkutano wa hadharani kwenye jimbo Tarime Vijijini.
Katika hatua nyingine Mbunge Lema amewataka viongozi wa Tanzania kuiga kwa Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta ambaye ameruhusu maandamano ya kumpinga.
"Rais Uhuru Kenyatta amewapa amri askari polisi Kuwalinda waandamanaji waliotaka kuandamana kupinga ushindi wake huu ni mfano wa kuigwa hasa ikizingatiwa hili linatokea katika nchi za Afrika Mashariki,".
Lema amewaomba viongozi wa dini kukemea kile alichodai kuwa ni udhalilishaji wa viongozi , pamoja na uvunjifu wa sheria za nchi .
Video Hii hapa play ushuhudie- VoA TV News

0 Comments:
Post a Comment