Halmashauri ya jiji la Arusha imevunja rekodi ya ukusanyaji wa fedha za mapato ya halmashauri hiyo kwa mwaka wa fedha 2016/2017 kwa malengo waliyokuwa wameyaweka ya kupata kiasi cha shilingi Billion 12.23 kwa mwaka wa fedha 2016/2017 na kukusanya kiasi cha shilingi Billion 13 ambayo ni sawa na asilimia 112% za ukusanyaji wa mapato hayo ikiwa imezidi zaidi kwa asilimia 12% za fedha hizo.
Akizungumza mbele ya Baraza la madiwani wa halmashauri ya jiji la Arusha mkurugenzi wa jiji hilo Bw Athuman Kihamia ameeleza kuwa halmashauri ya jiji la Arusha imeweza kuvuka malengo ya ukusanyaji wa mapato kutokana na utendaji mzuri wa serikali ya awamu ya tano.
Amesema kwamba makini na ushirikiano wa viongozi wa idara zote za halmashauri ya jiji hilo umeleta mafanikio hayo kwa haraka. Kuhusu matumizi ya mapato hayo , Mkurugenzi Kihamia ameeleza kuwa asilimia 68.9% ya mapato hayo zimeelekezwa kwa wananchi kwa ajili ya maendeleo.
Akizungumza mbele ya Baraza la madiwani wa halmashauri ya jiji la Arusha mkurugenzi wa jiji hilo Bw Athuman Kihamia ameeleza kuwa halmashauri ya jiji la Arusha imeweza kuvuka malengo ya ukusanyaji wa mapato kutokana na utendaji mzuri wa serikali ya awamu ya tano.
Amesema kwamba makini na ushirikiano wa viongozi wa idara zote za halmashauri ya jiji hilo umeleta mafanikio hayo kwa haraka. Kuhusu matumizi ya mapato hayo , Mkurugenzi Kihamia ameeleza kuwa asilimia 68.9% ya mapato hayo zimeelekezwa kwa wananchi kwa ajili ya maendeleo.

Amesema kuwa wananchi watarajie kuboreshewa maendeleo ikiwemo kuwajengea zahanati 5 katika kata mbali mbali za jiji, uboershaji wa vituo vya afya vilivyopo sambamba na ununuzi wa madawati na ujengaji wa madarasa katika baadhi ya shule za jiji .
Mkurugenzi huyo amewapongeza madiwani wote wa kata za jiji la Arusha mjini kwa jitihada zao za dhati za kimaendeleo na kuwataka wawe makini zaidi katika utendaji ili kuondoa hasara zisizo na ulazima kwa serikali na kubainisha kuwa zaidi ya shilingi miliini 14 zimekuwa hasara baada ya madiwani hao kuhairisha vikao hivyo pasipo ulazima wowote.
Akitoa maoni yake katika baraza hilo, Diwani wa Olasit Bw Alex Martini ameiomba serikali kumalizia miradi yote iliyoanzishwa mwaka 2016 / 2017 hasa katika kata yake kwani bado wananchi wanasubiri huduma hiyo ambayo ni haki yao sambamba na vituo vya afya.
Katika baraza hilo la mwisho wa mwaka wa fedha 2016/2017 madiwani wote wameweza kupitisha sheria/kanuni mpya zitakazo tumiwa kwa mwaka wa fedha ujao wa 2017/2018.
Sambamba na kanuni hiyo, kamati mpya za maendeleo zimeundwa ili kuleta ufanisi katika jiji pamoja na kufanya uchaguzi wa naibu meya wa jiji hilo. Katika uchaguzi huo, Bi Viola alipata nafasi ya kuendelea kukalia kiti chake kwa mwaka 2017/2018 kwa kupata kura 29 dhidi ya mgombea mwenzake Bw Abdulaswai Tojo aliyepata kura 3.





No comments:
Post a Comment