Thursday, February 6, 2014

MSHITAKIWA AMUUA POLISI ARUSHA




ASKARI Polisi F 5264, PC Sabato, (37) ameuawa kwa kupigwa jiwe kichwani na mtuhumiwa, Njoke Ole Kilimbi, (34)  wakati akimepeleka mahabusu kwenye gereza la Mkoa, Kisongo.

Tukio hilo limetokea JUMATANO WIKI HII mchana eneo karibu na hilo baada ya kushuka kwenye gari la abiria walilotumia ambapo walitembea umbali mfupi kabla ya kukutwa na dhahama hiyo ambapo aliokolewa na waendesha bodaboda.

Kamanda wa polisi mkoani hapa, Liberatus Sabas alithibitisha kutokea kwa tukio hilo ambapo alisema kuwa askari huyo alifariki juzi majira ya tano usiku wakati akipatiwa matibabu kwenye hospitali ya Mount Meru.

No comments:

Post a Comment