Monday, June 4, 2012

M4C YAVUNA 394 NGORONGORO

OPERESHENI Vua Gamba Vaa Gwanda imenikiwa kuvua  wanachama wa CCM 394 kutoka kata za Ngorongoro na enduleni  ambao jumapili walijiunga Chadema akiwemo  katibu wa UVCCM kata ya Enduleni, Cosmas Lakani.


 katibu wa CCM kata ya Enduleni akisubiri kuongea mara baada ya kumkabidhi kadi yake ya CCM mwenyekiti wa CDM mkoani Arusha, Mwigamba
Mpaka sasa jumla ya wanaccm 3,481 kutoka kata za Endulen na Ngorongoro wamejiunga na Chadema kwa kipindi cha mwezi mmoja tokea kuanzishwa kwa operesheni hiyo





Aliyekuwa katibu UVCCM Longido akitafsiri kwa kimaasai kile mwenyekiti wa CDM, Arusha, Samson Mwigamba alichoongea kwenye kata ya Ngorongoro.

wanakijiji wa kimba wakisubiri kadi zao za CDM ziandikwe majina


Afisa Mtendaji wa kata ya Ngorongoro, Beere akifuatilia mkutano huku akiwa amepata kilevi cha kutosha hivyo kuwa anapepesuka

 mmoja kati ya wanakijiji akiamua kumsindikiza afisa mtendaji baada ya kilevi kumzidi nguvu 

 Mwenyekiti wa BAVICHA, mkoa wa Arusha, Ephata Nanyaro akiongea kwenye kata ya Endulen


Mwenyekiti wa BAWACHA mkoani Arusha, Cecillian Ndossi akizungumza kwenye mkutano huo


wananchi wakifuatilia mkutano 




 katibu wa Chadema , Nuru Ndossi (mwenye gwanda)akifuatiatilia mkutano

No comments:

Post a Comment